UWEKEZAJI WA ZSSF UMELENGA UCHUMI WA KATI-SABRA

Image result for zssf

Mkurugenzi wa mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF Sabra Issa Machano amesema uwekezaji wa miradi ya kiuchumi unaofanywa na mfuko huo umelenga mpango wa serikali wa kuwa na uchumi wa kati.

Amesema awamu ya kwanza ya uwekezaji wa nyumba za kuishi za Mbweni umepata wateja na hivi sasa ZSSF inaendelea na mipango ya kutaka kujenga nyumba za kisasa za watu wa kiwango cha chini eneo la Kwahani.

Akizungumza na wajumbe wa baraza la wawakilishi juu ya marekebisho ya sheria ya mfuko huo huko Mbweni amesema uwekezaji huo unaendelea kuimarisha kifedha mfuko huo.

Sabra amesema kuanzia January hadi March mwaka huu mfuko umewalipa viinua mgongo mwanachama 242 zaidi ya shilingi bilioni 3.8 na shilling bilioni 2.4 za pencheni kwa wanachama elfu nane, 292.

Nao wajumbe wa baraza la wawakilishi wameuomba mfuko huo kuwaelimisha wananchi juu ya marekebisho ya sheria hiyo kutokana na kuwepo kwa malalamiko ya wanachama wake kukatwa mafao yao.

 

By Zanzibar Islamic News

WANIKAJI DAGAA KIHINANI KUPIGWA JEKI-DR. SHEIN

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shen ameutaka uongozi wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi kuwaangalia kwa karibu  wafanyabiashara wanaokausha dagaa katika eneo la Kihinani, ili kuona wanafanya kazi zao katika mazingira bora na salama.

Dk. Shein amesema hayo Ikulu ndogo Kibweni mjini Zanzibar, alipokutana na uongozi wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, ilipowasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Mpango kazi wa Wizara hiyo kwa kipindi cha Julai 2018 hadi mwezi Machi, 2019.

Alisema wafanyabiishara hao waliojikusanya na kujiajiri wamekuwa wakifanya kazi kubwa ya uzalishaji wa dagaa na kuuuza hadi nchi za nje, hivyo kuna kila sababu ya kuwaunga mkono, kuwatia moyo na kuwasaidia ili kuhakikisha wanafanyakazi katika mazingira bora na kuondokana na hatari ya kukumbwa na maradhi ya mripuko, ikiwemo kipindupindu.

Aidha, aliutaka uongozi huo kujenga mashirikiano ya karibu na Kampuni ya Uvuvi Zanzibar (ZAFICO) kwa kuzingatia kuwa Shirika hilo ni mali ya  serikali.

Alisema Shirika hilo lililoundwa kutokana an mtaji wa mashirika makuu matano ya serikali ni muhimu katika maendeleo ya Taifa na ustawi wa wananchi, hivyo kuna wajibu wa kulilea, sambamba na kufanikisha dhana ya Uchumi wa Bahari.

Dk. Shein aliukumbusha uongozi wa Wizara hiyo umuhimu wa kusimamia maazimio yaliofikiwa katika semina maalum kuhusiana na rasilimali ya mchanga iliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil, akibainisha umuhimu wake katika uhifadhi wa rasilimali za Taifa.

Aliitaka Idara inayohusika na rasilimali ya mchanga kusimamia vyema pamoja na kuhakikisha taratibu zote za upatikanaji wa rasilimali hiyo zinafuatwa.

Aliutaka uongzi huo kukijengea mazingira mazuri Chuo cha Kilimo Kizimbani ili kukiweka katika nafasi nzuri kuelekea mpango wa Serikali wa kukiunganisha na Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA).

Aidha, Dk. Shein aliupongeza uongozi na watendaji wa Wizara hiyo na ile ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji kwa kazi nzuri iliofanywa kufanikisha utekelezaji  wa majukumu yao katika kipindi cha miezi tisa iliyopita.

Nae, Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Mmanga Mjengo Mjawiri alisema katika kipindi hicho Wizara imepata mafanikio makubwa katika udhibiti wa matumizi ya mchanga kupitia Kamati ya Baraza la Mapinduzi.

Alisema utaratibu madhubuti uliowekwa umepelekea kuwepo matumizi sahihi ya mchanga kwa mujibu wa mahitaji, hivyo kuwa suluhisho la tatizo la kurundikana kwa mchanga.

Aidha, alisema Wizara hiyo ilishirikiana na Wizara ya Ardhi kuyatambuwa, kuyapima na kuyapatia Hati miliki maeneo ya kilimo ikiwa ni hatua ya kukabiliana na uvamizi wa maeneo ya misitu na kilimo kwa shughuli za makaazi ya watu na miradi mingine ya maendeleo.

Alisema Serikali kupitia Wizara hiyo ilitowa ruhusa ya kugawa mashamba ekari 732 yaliopo kisiwani Pemba ili  yaendelezwe kupitia shughuli za  kilimo na mifugo.

Vile vile, alise Wizara hiyo iliimarisha udhibiti wa matumizi ya raasilimali zisizorejesheka kwa kuandaa utaratibu maalum wa upatikanaji wa rasilimali hizo pamoja na kufanya doria shirikishi kwa kushirikiana na Vikosi vya SMZ .

Alisema katika kipindi hicho Serikali ilifanya kongamano la Sheria za Ardhi na hali halisi ya misitu na maliasili zisizorejesheka kwa lengo la kutoa elimu na kuihamasisha jamii juu ya umuhimu wa uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za Taifa.

Mjawiri alisema katika utekelezaji wa malengo yaliowekwa, pia Wizara hiyo ilikabiliana na changamoto za kuongezeka kwa bei ya pembejeo, matumizi mabaya ya misumeno, kuwepo kwa nzi wa matunda pamoja na kuwepo kwa mahitaji ya matumizi ya mchanga, huku maeneo ya uchimbaji yakipungua.

Alieleza azma ya kuziendeleza sekta zinazounda Wizara hiyo, kwa kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji maji, uchimbaji visima na mabwawa pamoja na mitaro ya Umwagiliaji maji kupitia mradi wa EXIM Bank wa Korea, utakaotumia hekta 500, sambamba na hekta 65 kupitia mradi wa ERPP

Aidha, alisema Wizara inalenga kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga pamoja na kushajiisha matumizi ya pembejeo kwa kununua na kusambaza mbolea, dawa ya kuuliya magugu pamoja na mbegu ya mpunga.

Wakati huo huo, akiwasilisha taarifa ya mpango kazi kwa kipindi hicho, Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Sira Ubwa Mamboya, alisema Wizara hiyo imefanikiwa kukamilisha ujenzi wa kilomita 28 za barabara mbali mbali Unguja na Pemba kwa kiwango cha Lami, ikiwemo Bara ya Ole – Kengeja yenye urefu wa kilomita 14.

Aidha, alisema Wizara hiyo imefanikiwa kuendeleza ujenzi wa jengo jiipya la abiria katika Uwanja wa Ndege  (terminal 111), kuendelea na ujenzi wa maegesho pamoja na msingi wa kupitisha maji katika eneo hilo.

Vile vile, alisema Wizara imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya uwanja wa ndege kisiwani Pemba.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

ZSTC KUIMARISHA VITALU VYA MICHE YA MIKARAFUU

Image result for miche ya mikarafuuShirika la biashara la taifa Zanzibar ZSTC limekabidhi hundi ya shilingi milioni tano kwa mkuu wa wilaya ya kaskazini b bw Rajab Ali Rajab kwa ajili ya uimarishaji  wa  miche ya mikarafuu.
Akikabidhi hundi hiyo huko Katika kitalu cha miche ya mikarafuu na viyngo kilichopo mwanakombo mkurugenzi masoko wa Zstc  Bw. Salum Abdalla kibe amesema
hatua hiyo ni kuunga mkono juhudi za serikali za kuwawezesha wananchi kuzalisha kwa wingi miche hiyo  na katika mazingira bora.
Amesema  ZSTC itaendelea kuwasaidia kifedha na vifaa wananchi wa wilaya mbali mbali ili kasaidia jitihada za wakulima wa karafuu.
Akitoa shukurani zake mkuu wa wilaya ya kaskazini  b bw Rajab  Ali  Rajab  amesema fedha hizo zitasaidia kufanikisha malengo ya kukiimarisha kitalu hicho ili kiweze kukidhi mahitaji ya wananchi wa wilaya hiyo wanaohitaji miche.
Naye mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Makame Mwadini silima amesema azma ya halmashauri hiyo ni  kuimarisha uzalishaji wa  miche kutoka laki moja hadi kufikia milioni moja
By Ali Muombwa

GOOGLE KUWEKEZA ZANZIBAR

Naibu Spika wa Baraza la Wawakilkishi Zanzibar  Mgeni Hassan Juma ameupongeza Ujumbe wa Mtandao wa Gogle kwa azma ya kutaka kuiweka Zanzibar katika Ramani ya Kimataifa na kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta ya Utalii.

Amesema ujumbe huo utaweza kuchukuwa picha sehemu za Utalii na kuziweka katika Mtandao jambo ambalo litaweza kuvitangaza Visiwa vyetu katika pembe zote za Dunia.

Ameyasema hayo huko katika Ukumbi wa Tume ya Mipango Zanzibar wakati alipokuwa akifunguwa Mkutano wa kujadili namna ya ushirikiano baina ya Tume ya Mipango na Mtandao wa Gogle katika kuendesha Mradi wa kukuza Utalii kwa Wananchi katika maeneo  mbalimbali.

Amesema Dunia inategemea shughuli za Mawasiliano katika masuala ya Kijamii,Kiuchumi,Kiutamaduni na kisiasa hivyo Serikali itashirikiana na ujumbe huo ili uweze kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia malengo yaliokusudiwa.

Aidha ameitaka Tume ya Mipango kuangalia zaidi misingi ya Sheria ili kuhakikisha maeneo yanayopigwa picha yameruhusiwa kwa mujibu wa sheria kwa faida ya sasa na kizazi kijacho.

punjAmesema hali hiyo itapelekea Zanzibar kujitangaza na kujuilikana aina ya Hoteli zilizopo,Vivutio vya Utalii,Mandhari na hali ya Usalama jambo ambalo litaiwezesha Zanzibar kukabiliana na ushindani wa Utalii na nchi nyengine za Visiwa.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar Juma Hassan Reli amesema wamemua kuingiza Watu wa Ulinzi na Usalama katika Kamati Kiongozi ili kuhakikisha Zanzibar inabaki kuwa salama.

Hata hivyo Reli amewaomba Wananchi kutoa Mashirikiano wakati kamati hiyo itakapopita katika maeneo mbalimbali ili Ujumbe huo uweze kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia malengo yaliokusudiwa

 

By Takdir Ali

DK. SHEIN AFUTARISHA WANANCHI WA MKOA WA KUSINI PEMBA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein amefutari pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba na kuwataka kuendeleza amani na utulivu uliopo nchini ili maendeleo zaidi yazidi kupatikana. 

Hafla hiyo ya futari iliyoandaliwa na Rais Dk. Shein kwa ajili ya wananchi wa Mkoa wa Kusini  Pemba ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ndogo Chake Chake, na kuhudhuriwa  na viongozi mbali mbali wa Serikali, dini, vyama vya siasa pamoja na wananchi wa Mkoa huo.

Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya Rais Dk. Shein, Mkuu wa Mkoa huo Hemed Suleiman alieleza kuwa amani na utulivu ndio msingi wa maendeleo hivyo kila mmoja anapaswa kuilinda na kuiendeleza kwa nguvu zake zote.

Alisisitiza kuwa maendeleo yote yaliopatikana nchini yametokana na kuwepo kwa amani na utulivu mkubwa ambayo ndio chachu ya mafanikio hayo na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuyakuza maendeleo hayo kwa kadri uwezo utakapopatikana.

Alhaj Dk. Shein aliwatakia Ramadhani njema wananchi wa Mkoa huo na kuwasisitiza kuutukuza mwezi huo mtukufu kwa kusoma sana Qur-an kwani ndio mwezi ulioshuka kitabu hicho kitakatifu.

Alhaj Dk. Shein aliwataka wananchi wa Mkoa huo kuendelea kushirikiana na kupendana sambamba na kuwa wamoja huku akiwataka kuachama na mambo yote yaliyokatazwa ndani ya mwezi huu na miezi mengineyo ili waendelee kupata neema za Allah.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kupambana na vitendo na matukio yanayovunja maadili ya dini ya kiislamu na ambayo hayapaswi kufanyika katika jamii ukiwemo udhalilishaji wa wanawake na watoto pamoja na matumizi ya dawa za kulevya ambayo hayaleti taswira nzuri katika jamii.

Pia, Alhaj Dk. Shein alisisitiza haja ya kuendelezwa na kudumishwa kwa usafi hasa katika kipindi hichi cha msimu wa mvua huku akieleza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kupambana na athari za mvua kwa Unguja na Pemba.

Pamoja na hayo, Alhaj Dk. Shein aliwashukuru wananchi wote waliohudhuria katika futari hiyo aliyowaandalia na kupongeza jinsi walivyoonesha upendo mkubwa kwake wa kukubali muwaliko wake huo.

Nao wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba wakitoa neno la shukurani kwa upande wao ambalo lililotolewa na Sheikh Mohamed Suleiman ambaye pia, ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Istiqama Pemba walieleza kufarajika kwao na futari hiyo maalum waliyoandaliwa na Rais wao na kueleza jinsi walivyoifurahia.

Wananchi wa Mkoa huo walieleza kuridhishwa kwao na juhudi kubwa anazozichukua Rais Dk. Shein kwa kuwapelekea maendeleo makubwa wananchi wa Zanzibar wakiwemo wa kisiwa cha Pemba ukiwemo Mkoa wao wa Kusini.

Sheikh Mohamed alieleza kuwa Rais Dk. Shein amekuwa akifuata sunna na fadhila za Mtume Mohammad (S.A.W) ya kuwafutarisha watu katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhan jambo ambalo limesisitizwa katika mwezi huu kutokana na fadhila zake.

Aidha, wananchi hao walitumia fursa hiyo kumuombea dua Rais Dk. Shein kwa ukarimu na upendo wake mkubwa aliyowaonesha wananchi hao pamoja na ukarimu anaoendelea kuwaonesha wananchi wote wa Zanzibar katika kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na katika kipindi chote cha uongozi wake.

Wakati huohuo, nae Mama Mwanamwema Shein kwa upande wake alishirikiana kikamilifu na viongozi wanawake wa kitaifa pamoja na wananchi wa Mkoa huo wa Kusini katika futari hiyo maalum aliyoianda Rais Dk. Shein.

Akitoa neno la shukurani Mshauri wa Rais Pemba Dk. Mauwa Abeid Daftari alitoa shukurani kwa Rais Dk. Shein kwa ukarimu wake anaoendelea kuuonesha kwa wananchi wake sambamba na kusisitiza umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Leo Alhaj Dk. Shein anatarajiwa kuungana pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba katika futari maalum aliyowaandalia.

 

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

ZANZIBAR KUONGEZA UZALISHAJI WA MPUNGA

Image result for zao la mpunga zanzibarZaidi ya shilingi billioni miamoja na 45 zinatarajiwa kutumika katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji maji kwa lengo la kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari waziri wa wizara ya kilimo mali asili mifugo na uvuvi mh: mmanga mjengo mjawiri amesema mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya mpango mkuu wa umwagiliaji maji zanzibar.
Amesema mradi huo utajumuisha ujenzi wa mitaro ya umwagiliaji ,mabwawa manne ,uchimbaji wa visima 49 pamoja na ,ujenzi wa maeneo ya kuanikia mpunga katika mabonde saba ya mpunga yaliopo unguja na pemba yakiwemo cheju,kinyasini,kilombero na makwararani .
Mh: mmanga amefahamisha kuwa kumalizika kwa ujenzi wa mradi huo kutaongeza maeneo yalio endelazwa ya umwagiliaji maji kwa asilimia 200kutoka hekta 810 zinazomwagiliwa kwa sasa hadi kufikia hekta 2334 baada ya kumalizika kwa mradi huo ifikapo 2021.
Aidha amefahamisha kuwa mradi huo utaweza kuongeza uzalishaji wa mpunga katika maeneo ya umwagiliaji maji kutoka tani 5400 kwa mwaka jana na kukadiriwa kufikia tani 24,384 kwa mwaka ifikapo 2021 ambao utatoa ajira ya moja kwa moja kwa wakulima zaidi ya 15000 baada ya kukamilika kwake.
By Mwatima Mussa-ZBC

MEMBE AKATAA KUZUNGUMZIA URAIS

Membe vs Magufuli

Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Tanzania Bernard Membe ambaye amekuwa akitajwa kuwa na mpango wa kugombea tiketi ya urais 2020 amesema jina lake si hoja mbele ya masuala ya kitaifa.

Membe ameyasema hayo nje ya jengo la Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam, alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu video iliyoenea mtandaoni ikimuonesha mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu nchini Rostam Aziz akizungumzia mjadala wa urais 2020 na kumshauri Membe asijitose kuwania nafasi hiyo ili Rais John Magufuli amalizie awamu ya pili.

Membe amewaambia wanahabari kuwa Rostam hapaswi kuzungumzia mambo yanayomhusu mtu mmoja mmoja na badala yake kutokana na nafasi yake kwenye jamii anatakiwa kuongoza mijadala yenye manufaa kitaifa.

“Napata kigugumizi mno kumjibu rafiki yangu Rostam, lakini Rostam ni mchumi na nitakutana naye nimshauri kuwa anafanya vizuri sana katika jamii ya Watanzania anapozungumzia masuala ya uchumi,” amesema Membe na kuongeza “Inabidi azungumze main issues (masuala makuu) ya nchi, siyo personal (watu binafsi), hizi tunaachia watu wa chini, kwa level (hadhi) yetu ni tunazungumzia masuala ya kitaifa ya uchumi. Kwanini uchumi wetu upo hapa ulipo, kwanini wafanyabiashara wadogo na wakubwa wanafunga biashara zao au zile alizozieleza kama economic distortions (upotoshaji wa kiuchumi) tunazijibu vipi.”

“Rostam ni mchumi hivyo angejikita katika eneo hilo… asijaribu kuwa Mkristo zaidi ya Warumi … Yeye (Rostam) ni mwenzetu sisi tumekatwa mkia, ukikatwa mkia hata ujitahidi vipi mkia wako utabaki kuwa mfupi.”

Membe pia amewataka wanasiasa kuzungumza vitu ambavyo vinaendana na dhamiri zao, ” …tuwe tunazungumza kitu ambacho binadamu anatuheshimu… Nimshauri tu Rostam akubali status (uhalisia) asijaribu kuwa mtoto mzawa wakati mimi na yeye ni watoto wa kambo.”

BBC

Thailand: Mtoto mchanga aliyezikwa hai aokolewa na mbwa

Ping Pong alionekana akibweka na kuchimba mahala alipokuwa amezikwa mtoto kwenye shamba katika kijiji cha Ban Nong Kham

Mbwa mmoja nchini kaskazini mwa Thailand amemuokoa mtoto mchanga aliyekuwa amezaliwa baada ya kuzikwa hai anayedaiwa kuzikwa na mwanamke mwenye umri mdogo.

Mwili wa mtoto huyo mchanga wa kiume unasemekana ulikuwa umezikwa na mama mwenye umri wa miaka , 15, ambaye alikuwa amewaficha wazazi wake ujauzito.

Mbwa kwa jina Ping Pong alionekana akiwa anabweka na kuchimba ardhini kwenye shamba katika kijiji cha Ban Nong Kham.

Mmiliki wake anasema aliposogelea mahali alipokuwa ndipo alipoona mguu wa mtoto mchanga ukitokezea juu ya ardhi.

Wanakijiji walimkimbiza mtoto hospitalini ambako madaktari walimuogesha na kutangaza kuwa alikuwa mzima wa afya.

Mmiliki wa mbwa Ping Pong , Usa Nisaikha, anasema mguu wa mbwa hake hauna nguvu baada ya kugongwa na gari.

Aliliambia gazeti la Khaosod : ” Ninamtunza kwasababu ni mwaminifu sanana kila mara huwa ananisaidia ninapokwenda shambani kuwahudumia mifugo wangu. Anapendwa sana na kijiji kizima.

Inashangaza.”

Mbwa Ping Pong amekuwa mlemavu wa mguu tangu alipogongwa na gari Haki miliki ya picha KHAOSOD

Mama yake mtoto huyo mchanga amekwishashtakiwa kwa kumtelekeza na kujaribu kumuua.

Panuwat Puttakam, afisa lkatika kituo cha Chum Phuang, alililiambia gazeti la the Bangkok Post kuwa sasa mama huyo anahudumiwa na wazazi wake pamoja na mtaalamu wa kisaikolojia.

Alisema anajutia matendo y

Wazazi wa msichana wameamua kumlea mjukuu wao

BBC

Daniel arap Moi aamrishwa kulipa faini kwa kunyakua ardhi

Bwana Moi alikuwa rais wa pili wa Kenya mwaka 1978 ambapo alihudumu hadi mwaka 2002.

Mahakama nchini Kenya imemuamuru rais wa zamani wa Kenya kulipa fidia ya dola milioni 1.06 kwa mjane ambaye alimchukulia ardhi yake kenyume cha sheria

Bwana Moi alinyakua ardhi ya heka 53 iliyokuwa mali ya mjane Susan Cheburet Chelugui, alisema Jaji.

Bwana moi alinyakua ardhi hiyo kinyume cha sheria miaka 36 iliyopita, lakini ilisajiliwa kwa jina la Bwana Moi mwaka 2007.

Mume wake Chelugui Noah Chelugui alikuwa chifu wakati wa utawala wa Bwana Moi.

Rais huyo wa zamani ambaye ndiye rais aliyekuwa mamlakani kwa muda mrefu zaidi , alishutumiwa na Bi Chelugui na mtoto wake wa kiume David Chelugui kwa kusajili ardhi ya familia yao kwa jina lake miaka miwili baada ya Bwana yake Bi Chelugui kufariki dunia.

Inasemekana baadae Bwana Moi aliiuza ardhi hiyo kwa kampuni ya utengenezaji wa mbao Plywood Limited.

Moi aliitawala Kenya kwa mkono wa chuma na alishutumiwa kwa ukiukaji wa haki za binadamu.

Kampuni ya Rai Plywood Limited iliwaeleza majaji kuwa ilinunua ardhi hiyo kutoka kwa Moi mnamo mwaka 2007 baada ya kufanya uchunguzi wa kina wa kisheria kuhusu ardhi hiyo.

Hata hivyo, Bwana Moi hakuweza kuipatia mahakama ushahidi wowote juu ya jinsi alivyopata ardhi, anasema mwandishi wa BBC Mercy Juma aliyepo Nairobi.

Jaji Anthony Ombwayo alisema Bwana Moi alikuwa na mienendo ya “isiyo ya kawaida, ukiukaji katiba, kutofuata utaratibu ” na “yenye dosari “.

Bwana Moi alikuwa rais wa pili wa Kenya mwaka 1978 ambapo alihudumu hadi mwaka 2002.

Alilitawala taifa hilo kwa mkono wa chuma na alishutumiwa kwa ukiukaji wa haki za binadamu.

Kutokana na shinikizo la kimataifa, aliruhusu uchaguzi wa vyama vingi mnamo mwaka 1992 ,uliotawaliwa na ghasia zilizosambaa nchini na madai ya wizi wa kura.

Uamuzi wa kesi ni muhimu kwa Kenya.

Kumekuwa na kesi nyingi za unyakuzi wa ardhi unaodaiwa kufanywa na viongozi wa ngazi ya juu wa serikali na wafanyabiashara matajiri kwa miaka mingi, lakini waathiriwa hawana utashi wala pesa za kukabiliana na wanyakuzi.

Ufisadi katika mfumo wa mahakama ni tatizo jingine kubwa. Wakati mzozo unapopelekwa mahakamani, kesi huzoroteshwa kwa miaka mingi.

Wengi wanamatumaini kuwa hukumu hii dhidi ya Bwana Moi itaonekana kama jaribio na kwamba itatuma ujumbe kwa watu kwamba hawawezi tu kuwa wananyakua ardhi tena za watu maskini.

BBC

KAMPUNI YA UJENZI YA UTURUKI KUWEKEZA ZANZIBAR

Balozi Seif Ali Idd

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikutana kwa mazungumzo na Ujumbe wa Viongozi Watatu wa Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Afya na Uwekezaji kutoka Nchini Uturuki hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Katika mazungumzo yao Kiongozi wa Ujumbe huo Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya huduma za Afya na Uwekezaji {KAYI} Bwana Batur Engin alimueleza balozi Seif kwamba Taasisi hiyo yenye Wafanyakazi 600 inatoa huduma katika Mataifa 200 Duniani.

Bwana Batur alisema Wahandisi wa Kampuni hiyo huendeleza kazi za Miundombinu ya Ujenzi wa Hospitali kubwa za kisasa zenye vifaa vya Teknolojia mpya unaofanywa katika mfumo wa ubia.

Alisema zipo Hospitali kubwa zilizojengwa katika Miji ya Paris Nchini Ufaransa, Istambul Uturuki yenyewe pamoja na Hospiatli Kubwa zilizopo Nchini Kenya zinazotarajiwa kukamilika Ujenzi wake hivi karibuni.

Mkurugenzi Mkuu huyo wa Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Afya na Uwekezaji alieleza pia Kampuni yake huendesha Miradi mengine ya Miundombinu katika Sekta ya Mawasiliano kwa ujenzi wa Viwanja vya Ndege, Bara bara Kubwa za Kisasa pamoja na Mahoteli Makubwa.

Alifahamisha kwamba mtazamo wa Kampuni yake kwa sasa umezingatia kuwekeza katika Visiwa vya Zanzibar Miradi zitakayoweza kutoa huduma katika Mwambao wa Afrika Mashariki pamoja na Ukanda Mzima wa Nchi za Sahara.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tayari inaendeleza Miradi mikubwa ya Ujenzi wa Hospitali ya Kisasa katika eneo la Binguni pamoja na mpango wa Ujenzi wa Bandari ya Mizigo katika eneo la Mpiga Duri.

Balozi Seif aliueleza Ujumbe wa Viongozi hao kutoka Uturuki kwamba Kampuni yao ina fursa ya kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika uimarishaji wa Ujenzi wa Hospitali hiyo inayotarajiwa pia kuwa na Kitengo cha Mafunzo ya Afya.

“ Inapendeza kuona Ujenzi wa Hospitali Kubwa ya Binguni inafanana na mtazamo wa Kampuni hiyo katika uimarishaji wa Miradi yake katika Huduma za Afya na Uwekezaji Vitega Uchumi”. Alisema Balozi Seif.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alifahamisha kwamba Serikali hivi sasa ina mtazamo wa uwepo wa Hospitali ya Kimataifa itakayolenga kutoa huduma kwa Watalii pamoja na wageni wanaoingia Nchini kwa safari za kimatembezi.

Balozi Seif alisema mtazamo huo umekuja kutokana na Zanzibar kwa sasa kuimarika katika Sekta ya Utalii inayoweza kuchukuwa nafasi ya kwanza ya Uchumi wake.

Alisema kuimarika kwa huduma za Afya katika Sekta ya Utalii kutaipa hadhi Zanzibar kurejea katika hadhi yake ya kutoa huduma mbali mbali za kibiashara ndani ya Bahari ya Hindi kama ilivyokuwa ikifanya karne nyingi zilizopita kutokana na mazingira yake ya kuwa kituo cha Biashara enzi hizo.